United Republic of Tanzania
Bodi ya Rufani ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu

Huduma Zetu

Tunatoa huduma huru, za uwazi na za kitaalamu zinazodumisha haki, uwajibikaji na kuimarisha imani ya umma.

1

Utatuzi wa migogoro

Utatuzi wa migogoro

2

Uamuzi wa Rufaa

"AAAB ina mamlaka ya kutoa uamuzi wa mwisho uliotolewa na mahakama ya ru...

Misingi Mikuu

Nini Kinaongoza Bodi ya Rufani ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu

UWAZI

Bodi itatekeleza shughuli zake na kuwasilisha maamuzi yake kwa namna iliyo wazi, inayoeleweka na yenye uwazi, kwa lengo la kuimarisha imani ya wadau na kukuza imani ya umma katika utekelezaji wa majukumu yake.

TAALUMA

Bodi itazingatia viwango vya juu vya umahiri, weledi, bidii na maadili katika utekelezaji wa majukumu yake, ili kuhakikisha utoaji wa huduma bora za usikilizaji na uamuzi wa rufaa.

UADILIFU

Bodi itadumisha uaminifu, uadilifu na maadili katika utekelezaji wa shughuli zake zote, kwa kuhakikisha kuwa maamuzi yake yanazingatia sheria pamoja na misingi ya haki ya asili (Natural Justice).

BILA UPENDELEO

Bodi itashughulikia na kuamua rufaa zote kwa haki, kwa kuzingatia usawa, bila upendeleo na kwa msingi wa ukweli na sheria, huku ikihakikisha kuwa kila upande unaohusika unapata fursa na utendewaji sawa kwa mujibu wa sheria.

UHURU

Bodi itatekeleza majukumu yake ya rufaa kwa uhuru na kwa kuzingatia usawa, bila kushawishiwa isivyostahili, kuingiliwa kisiasa au kuathiriwa na mgongano wa maslahi, kwa mujibu wa sheria na misingi ya haki ya asili.

UWAJIBIKAJI

Bodi itabaki kuwajibika kwa maamuzi yake, utekelezaji wa majukumu yake na matumizi ya rasilimali za umma, kwa kuzingatia viwango vya juu vya uwajibikaji, uadilifu na usimamizi bora wa rasilimali.

Dira

Kuwa chombo huru cha rufaa kinachoaminika na chenye ubora wa kipekee katika kuhimiza uhalali wa kisheria, uzingatiaji wa taratibu stahiki, haki, uwajibikaji na weledi.

 

Dhamira

Kulinda usawa na misingi ya haki katika taaluma ya uhasibu kwa kuhakikisha rufaa zinashughulikiwa kwa kutopendelea upande wowote, kwa uwazi na kwa wakati, hivyo kuimarisha uwajibikaji wa kitaaluma, utawala bora na kuendeleza imani ya umma.

Kauli Mbiu

Fusce sed tortor lobortis arcu porttitor ornare at ut mi. Phasellus bibendum, eros quis ornare ullamcorper, tortor diam suscipit elit, malesuada efficitur lorem ante eu lacus.

Machapisho

Sera
Tazama
Sheria
Tazama
Guidelines
Tazama
By-Laws
Tazama
Fomu
Tazama